Tuesday, February 7, 2012

UKIMYA WA KEISHA WAZUA HISIA MBALI MBALI KUTOKA KWA MASHABIKI WAKE


UKIMYA wa msanii wa muziki wa kizazi kipya Keisha, umeanza kuleta maneno mengi kwa wadau wa fani hiyo, huku wengine wakisema hawezi kurejea tena katika fani na kufanya vizuri kama miaka miwili iliyopita.

Chanzo cha habari kilichozungumza nampekuzi wetu  kilisema kuwa msanii huyo mwaka huu anaonekana kuchoka kufanya kazi hiyo ingawa kuna wimbo ambao anaundaa hivi sasa.

Chanzo hicho ambacho kiliendelea kusema kuwa maisha ya msanii huyu kwa sasa ni magumu mno kutokana na sababu mbalimbali za kifamilia ambazo zinamfanya kukosa muda wa kufanya muziki.

“Yaani kuna maswali mengi juu ya ukimya wa
Keisha, lakini baadhi ya watu wake wa karibu wanajua kila kitu, na mara ya mwisho nadhani ni mwaka jana nilisikia kwamba anaweza kuachana na tasnia hiyo na kufanya baishara,” kilisema chanzo hicho cha habari.

Hata hivyo mwandishi wa habari hizi alimtafuta Keisha, ili kuweza kuzungumza mawili matatu juu ya muziki wake, lakini hakupokea simu aliyopigiwa zaidi ya mara 50.

Mpekuzi wetu hakukata tamaa  kumsumbua msanii huyo na alipopokea simu alijibu kuwa anafanya mambo yake mengine lakini hawezi kuacha muziki.

No comments:

Post a Comment